MTIKILA AENDA MAHAKAMANI



Mwenyekiti wa Chama cha Demokratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila anatarajia kufungua kesi Mahakama Kuu ya Tanzania kupinga kuendelea kwa mchakato wa mabadiliko ya Katiba Mpya.


Mchungaji Mtikila akizungumza na gazeti hili alisema, madhumuni ya kufungua kesi hiyo ni mchakato huo kukiuka hatua mbalimbali muhimu wakati wa kuiandaa ikiwamo kutoa elimu kwa wananchi kipi wanatakiwa kukifanya kabla ya kutoa maoni.


“Nakwenda kufungua kesi hiyo, kutaka mchakato huu unaoendelea ufutwe na utupiliwe mbali, tunataka mchakato unaowashirikisha Watanzania wote, walio katika vyama vya siasa,makundi mbalimbali ya kiraia na madhehebu ya dini na wasio na makundi wala madhehebu,” alisema Mtikila




Aliongeza “Nilikuwa kimya najipanga, najua nitashinda sijajua Mwanasheria Mkuu wa Serikali ataniletea mawakili wangapi lakini nitampangua mmoja baada ya mwingine.” Mchungaji Mtikila alisema, endapo majaji wa mahakama hizo watakaoisimamia kesi hawatatenda haki kutokana na matakwa ya Serikali ya CCM atakata rufaa.

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright WORLD OF TODAY Published.. Blogger Templates
Back To Top