SIMULIZI YA WATOTO WALIO TENGANISHWA NA KUONYESHA ALAMA YA CHADEMA hii hapa

 






Dar es Salaam.Watoto hao walipewa majina ya Eliud na Elikana, walizaliwa Februari 20, mwaka jana mkoani Mbeya wakiwa wameungana huku mama yao Grace Joel (20) akiwa hana matumaini ya watoto hao kutenganishwa au kuendelea kuishi.
Grace alikata tamaa zaidi baada ya mume wake Erick Mwakyusa kumtamkia wazi kuwa hana shida na watoto walemavu kwa kuwa kwenye familia yao ya kina Mwakyusa hakuna walemavu.
“Nilishangaa, familia yangu kunitelekeza baada ya kugundua watoto wameungana, mume na familia yake walinitamkia wazi kuwa hawana shida na watoto walioungana, mume wangu alisema hawezi kuwalea kwa kuwa kwao hakuna watoto wenye ulemavu wa aina hiyo,” anasema.
“Siyo siri nilisijikia uchungu, sikuamini mume wangu angeweza kunifanyia hivyo;siyo yeye tu hata familia yao sikudhani kama wangenigeuka hivyo.
“Hospitali ya Kyela ndiyo iliyonipeleka kwenye Hospitali ya Rufaa Mbeya ambao nao walivyoona hali ya watoto wangu wakanishauri kuja Muhimbili.Sikuwa na uwezo wa kufika Muhimbili, nawashukuru sana madaktari wa Rufaa Mbeya, madaktari wa Muhimbili na hasa Serikali iliyonifuta machozi.
Leo hii siamini kama ninawashika watoto wangu kila mmoja akijitegemea, sina cha kuwalipa zaidi nawaombea kwa Mungu wale wote walionisaidia kwa njia moja ama nyingine.
Kauli ya kukataliwa na mumewe ilikuwa mwiba mchungu kwa Grace ambaye alihisi dunia yote imemgeuka, na hakuwa na msaada toka kwa familia ya mume wake na familia yake pia.
Akiwa kwenye hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya, Grace alikata tamaa kabisa kuwa watoto wake Elikana na Eliud ambao aliwazaa kwa njia ya operesheni wakiwa na kila tano na nusu, kama watapona. Muda wote mama huyo alijawa machozi machoni mwake kwa kuamini watoto wake wasingepona.
Watoto hao walikuwa na njia moja ya kutolea haja ndogo pia njia ya haja kubwa walikuwa wanatumia moja.
Februari 25 mwaka jana, Grace akiwa na watoto wake ambao alikuwa amewafunika kwa upande mmoja wa kanga, akiwa hana uwezo hata wa kuwanunuliwa maziwa, alipewa rufaa na kufikia kwenye Hospitali ya Muhimbili na kulazwa kwenye wodi ya watoto, wakiwa chini ya uangalizi maalumu.
Daktari Zaituni Bokhari ndiye aliyekuwa akiwahudumia kwa karibu watoto hao na kumwombea misaada kwa watu mbalimbali ambao walijitokeza kuwanunulia nguo, maziwa na vitu vingine vingi.
“Ilikuwa kazi kubwa kumfanyia ushauri Grace hadi akubaliane na hali halisi, alikuwa amekata tamaa kabisa, ni kama alichanganyikiwa. Kuna wakati alitaka kutoroka Hospitali na kuwaachaa watoto, lakini ilibidi tuwe naye karibu na kumpa moyo na kumwambia watoto wake watapona. Tunashukuru kwamba baadaye akili yake ilitulia soma zaidi..........

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright WORLD OF TODAY Published.. Blogger Templates
Back To Top