UKAWA WALILIA KICHWA CHA SOSPETER MUHONGO, DK SLAA aeleza kwa nini kikwete anashindwa kumwadibisha



Dar es Salaam. Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), umelitaka Bunge kuiwajibisha Serikali ikiwa Rais Jakaya Kikwete atashindwa kutekeleza maazimio ya Bunge ikiwamo kumng’oa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.


Wakizungumza hapa jana, viongozi hao walisema endapo Rais atashindwa kumwajibisha Profesa Muhongo, basi wabunge wao watawasilisha hoja na kushawishi wengine kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu na umoja huo utaitisha maandamano nchi nzima.


Mwenyekiti mwenza wa umoja huo, Profesa Ibrahim Lipumba alihoji kwa nini Rais Kikwete anasita kumwondoa Profesa Muhongo wakati Bunge lilishatoa maazimio.


Alisema Bunge linalowakilisha wananchi zaidi ya milioni 45 liliazimia uteuzi huo utenguliwe lakini akaelezea kushangazwa kwake na hatua ya Rais kusema bado anachunguza.


“Hivi Rais anachunguza nini, haliamini bunge? Kama anavyoteua mawaziri pia ana madaraka ya kutengua nafasi zao, sasa anasita nini wakati azimio la Bunge limemwelekeza. Kama Rais Kikwete atashindwa kumwajibisha Muhongo atakuwa ameshindwa kutekeleza moja ya maazimio ya Bunge na Ukawa utaliomba Bunge kuiwajibisha Serikali.”


Alisema hotuba aliyoitoa Jumatatu wakati akiwahutubia wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam, haijakidhi matarajio ya wengi kwani kuna maazimio hayajatekelezwa.


Profesa Lipumba ambaye pia ni Mwenyekiti wa CUF, alisema Rais amekataa kutekeleza azimio la kutaka mitambo ya IPTL itaifishwe na kutoa sababu ambazo hazina mashiko.


“Tangu mitambo ya IPTL imefungwa Taifa limepata hasara kubwa kwa sababu umeme unaouzwa ni wa gharama kubwa kuliko mitambo yoyote ya umeme inayotumika katika bara la Afrika, Taifa limeingia hasara kubwa, Rais aitaifishe,” alisema Profesa Lipumba.


Alisema katika hotuba hiyo Rais Kikwete alionyesha kuipendelea IPTL na kuikandamiza Tanesco wakati akielezea kuwa fedha za escrow zilikuwa mali ya IPTL.


Alitaka hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya wote waliohusika na ufisadi wa Akaunti ya Tegeta Escrow na wengine walionufaika nazo.


“Sheria ya maadili itungwe upya ili iweke uwazi wa mtu yeyote kuona taarifa ya mali za viongozi.”


Mbatia na Dk Slaa mwananchi

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright WORLD OF TODAY Published.. Blogger Templates
Back To Top