Babu; kinyozi anayemiliki magari 75



New Delhi. Mfanyabiashara Leonard Willoughby aliwahi kusema; ‘siku utakayoanza kuishi kwa kuifuata mipango yako unayopanga, kila kitu katika maisha yako kitabadilika kabisa.’ Inawezekana watu wengi wanaufahamu msemo huo, lakini Ramesh Babu anajitapa kuyatendea kazi maneno hayo.


Babu ambaye ni kinyozi bilionea pekee nchini India, anasema aliuchukua ushauri wa Willoughby na kuamua kuutendea kazi tangu siku ya kwanza alipousikia na kwamba maisha yake yalianza kubadilika.


Kwa mujibu wa Jarida la ‘Your story’ la nchini India, Babu amefanikiwa kuvuka vizingiti kadhaa vya umaskini hadi kufikia kuwa mmoja wa watu maarufu nchini humo akiwa na uwezo wa kununua gari aina yoyote anayoitaka.


Asema kuwa mwaka 1994 alinunua gari lake la kwanza aina ya Maruti, lakini aliendelea na kuhifadhi fedha kidogo kidogo alizokuwa anazipata hadi mwaka 2004, alipoanzisha kampuni ya kokodisha magari, ikiwa na magari saba wakati huo.


Hadi kufikia mwaka huu, kinyozi huyo amelinunua magari 75 kati ya hayo matano ni ya kifahari yakiwemo, Mercedes, BMW, Audi, mabasi kumi na lile analolipenda liitwalo Rollsw Royce.


Pamoja na utajiri huo mkubwa alionao Babu, bado anaendelea na kazi yake ya kinyozi. Akisimulia maisha yake ya awali, anasema kuwa alizaliwa katika familia masikini, baba yake alikuwa kinyozi na kwamba alifariki mwaka 1979 wakati Babu akiwa na miaka saba.


“Baba yangu alituachia biashara ya saluni Mtaa wa Brigade ambalo mjomba wangu alichukua akaanza kuiongoza. Anawa anatupa kiasi kidogo cha fedha. Tulikuwa tunakula chakula kimoja kwa siku ili tuweze kuishi tu,” anasimulia.


Anasema alipokuwa shule ya msingi, alilazimika kufanya kazi ili kuweza kujikimu kimaisha kwa kupata kiasi kidogo cha fedha.


“Nilikuwa nikibeba magazeti na chupa za maziwa na kitu kingine chochote ambacho kingeweza kupunguza ugumu wa maisha ya mama yangu. Hii ndiyo sababu ya kuhitimu masomo yangu,” anasema.


Baadaye alifanikiwa uendelea na masomo yake, jambo lililomfanya mama yake aanzishe ugomvi na mjomba aliyekuwa akisimamia duka baada ya kugoma kutoa fedha za matumizi.


“Ndipo nilipomwambia mama nitachukua saluni na kukiendesha mwenyewe. Hakupenda uamuzi huo kwa kuwa alifikiri nitaacha masomo, lakini nilianza kazi hiyo.


“Asubuhi nilikuwa saluni, jioni nilikwenda masomoni kisha usiku nilikuwa saluni tena na kufanya kazi hadi saa 7 usiku. Hivyo ndivyo nilivyoanza kuitwa kinyozi,” anasema. Read more..........

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright WORLD OF TODAY Published.. Blogger Templates
Back To Top