Mbunge ashtakiwa kumtusi mke wa Mugabe

 
Mugabe


Mbunge mmoja wa chama tawala nchini Zimbabwe anatarajiwa kufikishwa kortini kujibu mashtaka ya kumtusi mke wa Rais Robert Mugabe, Grace Mugabe.

Mbunge huyo Bw Justice Wadyajena anadaiwa kutumia “lugha ya matusi” dhidi ya mwanachama mwenzake wa chama tawala cha Zanu-PF aliyekuwa ameweka picha ya Bi Mugabe kwenye gari lake.

Kisa hicho kinatazamwa na wengi kama sehemu ya vizozo ya ndani ya chama kuhusu nani atamrithi Rais Robert Mugabe ambaye atatimiza umri wa miaka wa miaka 92 Februari.

Bw Wadyajena amenukuliwa kwenye nyaraka za mahakama kwamba alimwambia Jimayi Muduvuri: "Wewe ni mjinga sana, sawa na mama huyu wenu.” Atafikishwa kortini Victoria Falls.

Mke wa rais nchini Zimbabwe huitwa "amai", maana yake mama, na wafuasi wa chama cha Zanu-PF.

Mbunge huyo amekanusha madai hayo.BBC
 
 

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright WORLD OF TODAY Published.. Blogger Templates
Back To Top