What the World Thinks About Clinton vs. Trump

Viewpoints: What the World Thinks About Clinton vs. Trump



Just a few months ago Hillary Clinton battling Donald Trump in the general election was unthinkable. Now it seems that anything is possible. To many Americans, Clinton vs. Trump is a choice between a government insider vs. an outsider. And nobody loves an underdog more than the American people. But what does the rest of the world think?

Worldpress.org has gathered a sampling of recent news coverage from around the globe to give you the international perspective on Hillary Clinton vs. Donald Trump.

Argentina – Buenos Aires Herald, March 2: Republican Donald Trump and Democrat Hillary Clinton took big steps toward securing their parties' presidential nominations yesterday with a series of state-by-state victories, but their rivals…aim to knock them off their pedestals in contests ahead in Michigan, Florida and Illinois.…"The stakes in this election have never been higher and the rhetoric we’re hearing on the other side has never been lower," Clinton told supporters in Miami. "Trying to divide America between us and them is wrong, and we’re not going to let it work." …At a news conference in a chandeliered ballroom at his seaside Mar-a-Lago resort in Palm Beach, Florida, Trump, who has never held public office, dismissed furious criticism aimed at him by establishment Republicans.…"I’m going to get along with Congress, okay? Paul Ryan, I don’t know him well, but I’m sure I’m going to get along great with him. And if I don’t, he’s going to have to pay a big price, okay?" Trump said in remarks that could further inflame party tensions.

China – Xinhua, March 3: "The big victories by Clinton and Trump mean in all likelihood that each will be their party's nominees for the general election," Brookings Institution's senior fellow Darrell West told Xinhua."These individuals have substantial leads over opponents and are in a great position to wrap things up by the end of March. Unless someone else runs as an independent candidate, this is likely to be the voter choice for this fall." …Trump has beaten analysts' predictions again and again. While just six months ago, no one expected him to clinch the Republican nomination, that scenario now looks increasingly possible. And while just a couple of months ago analysts thought he could never beat Clinton in the general election, now analysts say he can.

Lebanon – The Daily Star, March 3: One evening last June, some of the Republican Party’s wealthiest donors gathered for a cocktail party at an exclusive resort in Deer Valley, Utah, during a three-day retreat hosted by former Massachusetts Governor Mitt Romney.They had just heard from six presidential hopefuls. Tom Duncan, the CEO of tool-maker Positec Tool Corp, chatted with a few attendees about a fantasy ticket to secure the White House in November 2016: Wisconsin Governor Scott Walker, with Senator Marco Rubio of Florida as his running mate. ...No one mentioned Donald Trump, even though he had been signaling for months that he planned to run. Four days later, the New York property magnate declared his candidacy and within weeks had shot to the top of the polls, eclipsing all of his Republican rivals. … Republican donors, strategists and campaign operatives interviewed by Reuters admitted they had misjudged the mood of voters who have thrown their support behind Trump after he promised to build a wall on the Mexican border, temporarily ban Muslims from entering the United States and block Syrian refugees because they might be militants.

France – France 24, March 2: Senior Republicans are running out of options in their race to stop the Donald Trump bandwagon. Whether or not they succeed, the battle is likely to prove costly for the Grand Old Party. … Josh Kraushaar, a political editor at the National Journal… noted that while Trump’s poll ratings are on the upswing, surveys also show that a quarter of the Republican electorate “won’t vote for him under any circumstances,” while some would even cross over to the Democrats, provided they pick a moderate like Clinton. … “The emerging scenario in Washington is that the Republicans are going to take this to a contested convention,” Kraushaar said, suggesting an ugly showdown between the pro- and anti-Trump camps was a likely outcome. “If Trump doesn’t come out as the nominee his supporters are going to be furious, but if he does then you have about a quarter of Republicans who won’t vote for him,” he said, describing the conundrum as a “no-win situation.”

Germany – Deutsche Welle, March 2: Political Berlin hasn’t really come to grips with the possibility that Donald Trump’s next visit here could be in his capacity as US president because it’s a scenario no one wants to contemplate, says DW’s Jens Thurau. … The idea of Russia and the United States cozying up to one another with Germany caught in the middle is enough to make anyone afraid. …For months now, German politicians have been looking across the Atlantic with a mixture of fascination and horror. The hair! The aggression! The crude rhetoric! … And doesn't all this with Trump seem surreal, like something dreamed up in Hollywood? And if it should become real, what then? But no, that's not something anyone really wants to consider just yet.

Iran – Fars News Agency, March 3: The number of Google searches on how to immigrate to Canada from the United States spiked several times on Wednesday as presidential candidate Donald Trump swept the US Republican primaries. According to a tweet by Google's data editor Simon Rogers, Google searches for "how can I move to Canada?" increased by 350 percent over four hours after Trump's victory in seven states was announced. Most of the searches were detected in Massachusetts, where Trump won 49 percent of the vote, Sputnik reported. Analysis by tech website Mashable revealed that by midnight the "Canada-moving" search had increased by 1,150 percent.

Israel – The Jerusalem Post, March 4: A letter posted Wednesday by some 60 influential conservatives in think tanks and alumni of Republican administrations lists the ways they say the billionaire real estate magnate would “make America less safe,” including “hateful, anti-Muslim rhetoric” that “undercuts the seriousness of combating Islamic radicalism.” It also accuses him of contempt for neighbors such as Mexico and allies like Japan while admiring dictators like Russia’s Vladimir Putin. The letter says Trump is feckless. “He swings from isolationism to military adventurism within the space of one sentence,” it said.

United Kingdom – The Guardian, March 5: Barring an unforeseen disaster on either side, Clinton and Trump are now on a collision course for the presidential election on 8 November 2016. The bombastic, swaggering, sometimes vulgar billionaire has stunned the political world, plunged the Republican Party into civil war and, among the pundit class, relegated the prospect of the 240-year-old republic’s first female president to a footnote. … The outside world, overjoyed by the election of America’s first black president just eight years ago, is asking: how did it come to this? …One chilling statistic for Clinton stands out: more than 8 million voters took part in the Republican Super Tuesday contests, while the Democratic turnout was around 5.5 million. … Clinton is compared to Bill Clinton and Barack Obama; Trump is compared to everyone from Benito Mussolini to Juan PerĂ³n to Silvio Berlusconi.

Canada – The Star, March 5: Let the righteous hand wringing stop. Let the sanctimonious hypocrites of America’s political and media class cease. And, above all, let us not delude ourselves about why a vulgar, bullying and racist Donald Trump has come to dominate U.S. politics. The answer is simple. The allure of easy money is what now drives America’s corrupt democracy, perhaps irreparably. It takes the form of an unholy alliance linking many American politicians, the billionaires who own them and the U.S. broadcast news media that has sold its soul for the massive profits they are reaping. … A key lesson of the past hundred years is that democracies do die. On behalf of our American friends, and the rest of us, let’s hope the Trump reality show soon comes to an end.

Australia – The Age, March 3: For about a quarter of a century, she has been vilified as loudly as she has been lionized, told that her talents pale beside her husband's, called "likable enough" but seldom lovable, and cast in supporting roles: the first lady, the secretary of state. She never retreated. Never gave up. … Let's give her this moment, because she fought her way here. She tuned out the naysayers. She turned a blind eye to all her scars. Her ability to do that may reflect unrestrained ambition, a sturdy confidence in her mission or - more likely - an intricate cat's cradle of both. Whichever the case, it demonstrates a grit that could be her greatest asset in a general election. Clinton has the toughness to engage in - and survive - a brutally ugly contest. She also has the smarts to know the cost of it. Has she honed the character and nimbleness to prevail in a more inspiring, unifying way? As well as we know her, this is yet to be revealed.

Pakistan – Dawn, March 5: Last week, former CIA director Michael Hayden said in an interview to a US media outlet that the American military would refuse to obey Mr. Trump if he gets elected and orders them to torture prisoners or kill the families of terrorists. … At the [Thursday] debate, a moderator, Bret Baier, asked Mr. Trump to comment on Gen Hayden’s statement. Mr. Trump rejected the suggestion that the US military would defy their president. … “What would these animals over in the Middle East, that chopped off heads think of a hesitation to commit war crimes?” Mr. Trump asked. “We should go for waterboarding and we should go tougher than waterboarding.” … The remarks earned him a wild applause from the audience.

Taiwan – China Post, March 3: Increasingly, leading Republicans talk of a contested convention in July as their best remaining option for stopping Trump, whose divisive rhetoric about immigrants and ethnic and religious groups has some fearing a Republican wipeout in November. … Speaking from his gold-flecked Mar-a-Lago resort, Trump asserted that his candidacy is a "movement" and he claimed he would unify the party by training his fire on Clinton.worldpress

Haikuwa rahisi kufunga ndoa na Dk Slaa, aeleza mwana ndoa mpya wa Dk slaa

JIBU ALILO LITOA MGABE BAADA YA KUULIZWA SWALI NA MWANDISHI WA HABRI

 Mugabe


Kiongozi wa muda mrefu wa Zimbabwe Robert Mugabe amejibu kwa mzaha swali kuhusu mrithi wake na kusema bado anaweza kurusha ngumi.

Rais Mugabe aliulizwa nani atakayemrithi wakati wa sherehe ya kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa.

Kiongozi huyo ambaye amekuwa uongozini tangu 1980 ametimiza umri wa miaka 92.

"Mbona unamtaka mrithi?" alimwuliza aliyekuwa akimhoj



“Unataka nikutwange ngumi uanguke chini ndipo uamini kwamba bado nina nguvu?”, gazeti la serikali ya Herald limemnukuu.

Bw Mugabe, alisema hatastaafu katikati mwa muhula wake wa sasa, ambao ulianza 2013.


 


Mbunge ashtakiwa kumtusi mke wa Mugabe

 
Mugabe


Mbunge mmoja wa chama tawala nchini Zimbabwe anatarajiwa kufikishwa kortini kujibu mashtaka ya kumtusi mke wa Rais Robert Mugabe, Grace Mugabe.

Mbunge huyo Bw Justice Wadyajena anadaiwa kutumia “lugha ya matusi” dhidi ya mwanachama mwenzake wa chama tawala cha Zanu-PF aliyekuwa ameweka picha ya Bi Mugabe kwenye gari lake.

Kisa hicho kinatazamwa na wengi kama sehemu ya vizozo ya ndani ya chama kuhusu nani atamrithi Rais Robert Mugabe ambaye atatimiza umri wa miaka wa miaka 92 Februari.

Bw Wadyajena amenukuliwa kwenye nyaraka za mahakama kwamba alimwambia Jimayi Muduvuri: "Wewe ni mjinga sana, sawa na mama huyu wenu.” Atafikishwa kortini Victoria Falls.

Mke wa rais nchini Zimbabwe huitwa "amai", maana yake mama, na wafuasi wa chama cha Zanu-PF.

Mbunge huyo amekanusha madai hayo.BBC
 
 

Samia, Majaliwa watumia ndege za kukodi


magufulu akiwa na majaliwa na samia suluhu

MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wamelazimika kutumia ndege za kukodi baada ya ndege za Serikali kuharibika.

Wiki iliyopita, Samia alilazimika kutumia ndege ya kukodi alipofanya ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Tanga.

Pia Waziri Mkuu katika ziara zake mbalimbali amelazimika kutumia ndege za kukodi.

Wiki chache zilizopita, Majaliwa alitumia ndege ya kukodi kwenda mikoa ya Iringa na Mtwara na jana aliwasili mkoani Mwanza kwa ziara ya siku 14 katika mikoa ya Kanda ya Ziwa ambapo pia alitumia ndege ya kukodi.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA), Kapteni Kenan Mhaiki, alikiri ndege mbili za Serikali ambazo zimekuwa zikitumiwa na viongozi mara kwa mara kuwa ni mbovu.

Alizitaja ndege hizo ambazo kwa kawaida viongozi huzitumia katika shughuli za kawaida ndani ya nchi kuwa ni Fokker 50 na Fokker 28 (5H-CCM).

“Ndege zipo zinafanyiwa matengenezo, moja inahitaji matengenezo ya juu zaidi na nyingine inasubiri tu vipuri kutoka nje,” alisema Mhaiki.

Alisema hadi sasa ndege za Serikali zipo tatu, ikiwamo ya rais aina ya Gulfstream Aerospace (5H-One) ambayo anatumia sasa.

Alipotafutwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profsea Makame Mbarawa, alisema: “Suala hilo naweza kulizungumzia nikiwa Dar es Salam… niko kwenye mkutano nivumilieni.”

Mwanzoni mwa mwezi uliopita, Rais Dk. John Magufuli wakati akizungumza katika uzinduzi wa Mwaka wa Mahakama na Siku ya Sheria nchini, alisema kesi 442 zinazohusu wakwepa kodi endapo zitaamuliwa zitaiingizia Serikali Sh trilioni moja, fedha ambazo Read more...

Mdee: Watake wasitake Dar wataachia

Halima Mdee


 MBUNGE wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), amesema sasa umefika wakati kwa polisi kuacha kutumika, huku akituma salamu kwa viongozi wa CCM, akisema watake wasitake wataachia Jiji la Dar es Salaam liongozwe na Ukawa. Kauli hiyo aliitoa jana Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kukamatwa kwake, muda mfupi baada ya kuachiwa kwa dhamana. Alidai kitendo cha kuwekwa ndani hakitawazuia kufanya kazi zao, na pia alilitaka Jeshi la Polisi kufuata taaluma za kazi zao kwa kuwa kufanya kazi kwa kufuata maagizo ni upuuzi. “Kosa hili ni la kipuuzi, polisi waache kutumika,” alidai na kuongeza kwamba Rais Dk. John Magufuli ajiandae kuongozwa na Ukawa atake asitake kwa sababu namba hazidanganyi. Jana Mdee pamoja na Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara, walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu shitaka la kumjeruhi Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam (RAS), Theresia Mmbando. Halima (37), Waitara (40) na mfanyabiashara Rafii Juma (21) pamoja na Diwani wa Kata ya Kimara, Ephrein Kinyafu (33), walifikishwa mahakamani hapo jana na kusomewa mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi. Kabla ya kusomewa mashtaka, mawakili wa Serikali, Faraja Nchimbi, akishirikana na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi na wakili mwingine wa Serikali, Mwanaamina Kombakono, waliiomba mahakama kutoa hati ya wito kwa mshtakiwa wa nne Diwani wa Kata ya Kimanga, Manase Njema (56) ili aweze kusomewa shtaka Mwanaamina alidai washtakiwa hao walitenda kosa hilo, Februari 26, mwaka huu katika Ukumbi wa Karimjee wilayani Ilala, Dar es Salaam. Ilidaiwa washtakiwa hao walimjeruhi Theresia na kumsababishia majeraha. Washtakiwa hao walikana mashtaka, ambapo upande wa Jamhuri ulidai upelelezi haujakamilika na kuomba shauri hilo kuahirishwa hadi tarehe nyingine kwa kutajwa. Mdee na wenzake walikuwa wakiwakilishwa na jopo la mawakili likiongozwa na Wakili Peter Kibatala. Wengine ni John Mallya, Fredrick Kiwelo, Hekima na Omary Msemo. Kibatala aliiomba mahakama kuwapatia dhamana washtakiwa kwa masharti nafuu ikilinganishwa na kosa lenyewe. Akitoa masharti ya dhamana, Hakimu Shaidi alisema kila mshtakiwa atajidhamini mwenyewe na kutia saini ya dhamana ya Sh milioni mbili. Alisema hati ya wito wa kufika mahakamani kwa mshtakiwa Njema itolewe. Mdee na wenzake walitimiza masharti hayo ya dhamana na kuachiwa hadi Machi 16, mwaka huu kesi itakapotajwa. Jana, viongozi wa Chadema na baadhi ya wanachama walifurika mahakamani hapo kwa ajili ya kufuatilia kesi hiyo. Baada ya kuachiwa kwa dhamana, Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, Salum Mwalimu, Mdee na Waitara walizungumza na watu waliokuwapo mahakamani hapo. Mwalimu alionya kwamba Serikali isithubutu wala kujidanganya kwamba itawaweka watu wao ndani ili waweze kuitisha mkutano wa Uchaguzi wa Meya wa Jiji la Dar es Salaam ambao umekwama kufanyika mara tatu kutokana na mvutano uliopo.

Rais Kikwete, Mkapa na Makongoro Nyerere Waishambulia UKAWA kwa zamu......Magufuli Aahidi Kuwashughulikia Mafisadi



Rais Jakaya Kikwete, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa na Mtoto wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, Makongoro Nyerere wameshambulia vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA). 


Wakizungumza kwa zamu katika Uwanja wa Jangwani jijini Dar es Salaam wakati wa kufungua kampeni za chama hicho wamesema, mgombea wa UKAWA hana sera za wapinzani. 


Katika mkutano huo uliotawaliwa na vijembe kwa UKAWA Rais Kikwete bila kutaja jina amesema, katika umoja huo kuna mgombea anayesimama kama mgombea binafsi kwa kuwa, sera zake ni tofauti na chama anachosimama kugombea. 


Alikwenda mbali na kuonesha kushangazwa kuwa, mmoja vyama viwili ambavyo sio msingi wa chadema ndio vimesimama katika ngazi ya urais na mgombea mwenza wake. 


Rais Kikwete aliwalenga Mgombe Urais wa Chadema, Edward Lowassa aliyejiunga na chama hicho akitokea CCM pamoja na Juma Duni Haji aliyejiunga na Chadema akitokea Chama cha Wananchi (CUF). 


“Wagombea sio wa Chadema. Mmoja ni CCM na mmoja ni CUF.., Pale kuna mgombea urais ambaye unaweza kusema kama mgombea binafsi maana ana sera zisizofanana na chama,” amesema Rais Kikwete na kuongeza “lakini wameyataka wenyewe.” 


Hata hivyo Kikwete hakumwacha Waziri Mkuu Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Frederick Sumaye aliyejiunga na chama hichi siku moja iliyopita. 


Kikwete amesema, pamoja na Sumaye kujieleza lakini hakumwelewa alichokuwa akikusudia “nimejaribu kusikiliza anasema nini lakini sikuelewa kabisa,” amesema. 
Hata hivyo amesema, CCM haikubahatisha kumteua Dk John Magufuli kuwa mteule wa chama hicho katika urais na kwamba, “tumemweka kwa sifa zake, tunataka rais anayeipenda nchi na anayependa wananchi wa nchi hii.” 


“Magufuli anayo sifa hiyo. Tumesema, hatutaki kuchukua mgombea mwenye makando kando mengi na tukatumia muda wetu mwingi kujitetea sisi na yeye kabla ya kuomba kura. Tunamtaka mgombea mwaminifu, mwadilifu. Safari hii Mungu kamchagua Magufuli.” 


Kabla ya Rais Kikwete kuzungumza, alitanguliwa na Mkapa ambaye amesema, kuna vyama vinawadanganya Watanzania kuwa wanawatafutia ukombozi-wapumbavu. 


“Kuna chama kimoja tu cha ukombozi hapa Tanzania, ni CCM iliyotokana nas ASP na TANU. Kuna vyama vinawadanganya Watanzania eti wanataka kuwakomboa wananchi-wapumbavu, nenda nchi zote za jirani uliza chama cha ukombizi Tanzania watakwambia CCM. Nina kila sababu ya kusema wapumbavu,” amesema. 


Hata hivyo amesema, haitoshi kusema mtu anauchukia umasikini peke yake. 


“Haitoshi kusema unauchukia umasiki, lazima useme unauchukiaje umasikini?” amesema Mkapa. 


Lowassa katika hotuba zake mbele ya wananchi kwenye safari zake za kutafuta wadhamini alipokuwa CCM na hata baada ya kuhamia Chadema, amekuwa akisema anauchukia umasikini-haupendi. 


Hata hivyo Mkapa amesema, timu ya CCM ni madhubuti kwa kuwa Magufuli anapenda kushirikiana na wenzake, yupo mstari wa mbele katika kutekeleza mambo yote ya umma na kwamba, wakati wote ni mfano wa tabia nzuri kwa vitendo vyake. 


Makongoro ndio aliyefungua ukurasa wa mashambulizi kwa UKAWA kwa kumvaa Sumaye baada ya kujiengua CCM. 


Makongoro amesema, anamshangaa Sumaye aliyejiunga na vyama vinavyounda UKAWA na kwamba, alipaswa kukubali matokeo ya kushidwa 


Makongoro alianza kwa kibwagizo “kuna mmoja-au niache?- kuna yule kaka yangu mmoja nasikia afya yake sio kweli. Kuna huyu mwingine wa jana (Sumaye)? 


“Sumaye tumpige kanzu au tumuache hivihivi, kwani angetulia tungeshughulika naye, kajileta mwenyewe sasa mimi nifanyeje, nimpige tobo?” amesema na kuongeza; 


“Sumaye akiwa Waziri Mkuu na kaka yangu Kikwete (Rais Kikwete) waliingia kwenye tano bora, Sumaye alikuwemo, kura zake hazikutosha zikatosha za Kikwete, kwa kuwa aliingia tano bora akasema, chama kizuri. 


“Miaka 10 baadaye tano bora hakuingia- Sumaye akatuambia mkimpa Lowassa kugombea urais hiki chama mimi nitahama, sasa huyo ni mkweli ama muongo. Hii ndio shida ya kusema uongo, kusema rahisi kuukumbuka tabu,” amesema Makongoro. 


Katika mkutano huo, mgombea mwenza wa CCM, Samia Suluhu Hassan amesema, atasimamia na kuwawezesha akina mama. 


Pia ameahidi kusimamia pesa Sh. Mil 50 zinazotolewa na serikali kwa ajili ya kupelekwa vijijini. 


“Nitasimamia kuwawezesha akina mama, pesa za vijijini Sh. Mil 50 zitatoka kwa ajili ya vijijini nitazisimamia. Mimba za utotoni nitasimamia kuhakikisha zinaondoka, pia nitahakikisha maji yanapatikana na kusaida akina mama wote,” amesema. 


Akizungumzia uzowefu alioupata amesema, amekuwa karibu na Makamu wa Rais wa sasa, Dk. Mohammed Gharibu Bilal hivyo hakuna wasiwasi katika nafasi hiyo. 


“Nilikuwa kwenye mikono mizuri ya Dk. Bilal, najua kazi zilivyo nawahakikishia Ofisi ya Makamu wa Rais itasiamama vyema kutekeleza ilani ya uchaguzi pamoja na muungano,” amesema. 


Dk. Magufuli amewaahidi watanzania kujikita katika kutetea maendeleo ya wananchi kwenye Nyanja zote. 


Dk. Magufuli amesema utawala wake utajikita katika masuala ya kilimo, afya, uchumi na amani ya nchi. 


“Watanzania natambua mnapenda kuona mabadiliko, nitasimama vizuri katika miradi ya uchumi. Watanzania nawahakikishia shida na matarajio yenu nayajua, nayafahamu na natambua ninao uwezo wa kuyashughulikia. 


"Mnataka suala la rushwa, wizi serikalini vikomeshwe haraka. Kwa kuwa palipo na rushwa ufisadi hakuna maendeleo, nitasimamia hilo,” amesema. 


Amesema, kama atachaguliwa “nitahakikisha naunda mahakama maalumu ya kushughulikia mafisadi na majizi yafungwe haraka.”

JK ahaha kupata ushauri


Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Mrisho Kikwete
Dodoma. Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete alilazimika kutafuta ushauri kutoka kwa watu mbalimbali kwa ajili ya kuwezesha kazi ya mchujo wa wagombea urais kuisha salama, chama hicho kilisema jana.


Kikao cha Kamati Kuu, ambacho ratiba ya awali ilionyesha kingefanyika Julai 9, hakikuweza kufanyika kama ilivyopangwa na badala yake kilifanyika jana jioni mpaka usiku, hali iliyosababisha vikao vingine kuchelewa kuanza pia.


Akizungumza na waandishi wa habari jana, katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema mwenyekiti huyo alikuwa akitafuta ushauri kwa watu mbalimbali na ndio maana vikao hivyo vya juu havikuweza kufanyika katika muda uliopangwa.


Nape alisema sababu nyingine ya kuchelewa kwa vikao hivyo ni shughuli za chama na Serikali alizokuwa akizifanya Rais Kikwete, ambaye juzi alizindua ukumbi mpya wa chama hicho na baadaye mchana alihutubia Bunge kwa ajili ya kulivunja.


“Mwenyekiti alikuwa na vikao mbalimbali vya consultation (mashauriano) na wadau ili kuhakikisha vikao vinakwenda salama,” alisema Nape.


Hata hivyo, Nape hakuelezea vikao vya mashauriano kati ya Rais Kikwete na Serikali vilihusisha makundi gani.


Lakini Rais Kikwete kwa mujibu wa Katiba ni Amiri Jeshi Mkuu na pia ndiye mwenyekiti wa Kamati ya Usalama ya Taifa inayohusisha majeshi yote na wadau wengine.


Hata hivyo, kumekuwa na minong’ono mingi kwamba baadhi ya kambi za wagombea wenye nguvu na ushawishi zilikuwa zikiendelea na vikao usiku kucha kwa ajili ya kuweka mikakati ya jinsi ya kufanikisha azma za wagombea wao.


Licha ya kambi hizo pia kumekuwa na makundi ya wapambe wa wagombea waliojazana katika maeneo mbalimbali ya mji wa Dodoma, kwa kila kundi kutambia kundi jingine kwamba lazima washinde kwa namna yoyote, hali iliyoonekana kuashiria uwezekano wa kutokea uvunjaji wa amani.


Polisi wamekuwa wakifanya doria kwenye maeneo yenye baa kwa ajili ya kuwalazimisha wamiliki kufunga sehemu hizo za biashara kwa mujibu wa muda uliowekwa kisheria.


Kwa mujibu wa ratiba ya awali iliyotangazwa na Nnauye, Kamati ya Maadili na Usalama ya Taifa ilikuwa ifanyike Julai 8 na kufuatiwa na Kikao cha Kamati Kuu (CC) Julai 9 na kisha kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa jana na kufuatiwa na mkutano mkuu leo na kesho.


Kutokana na sababu hizo, Nnauye alisema Kamati ya Maadili na Usalama na CC vingefanyika jana kabla ya NEC kukutana leo na kuendelea na Mkutano Mkuu.read more............

TASWIRA MBALIMBALI KUTOKA KWENYE MKUTANO MKUU WA CCM MJINI DODOMA USIKU WA JANA.



Meza Kuu ikiongowa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete tayari kwa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi unaoendelea usiku huu kwenye Ukumbi wa Mikutano wa CCM wa Dodoma Convition Centre, uliopo njia ya Kuelekea Chuo Kikuu cha UDOM, Mjini Dodoma.* *Mwenyekiti wa CCM, Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Aliekuwa Mgombea Urais na Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Edward Lowassa wakati alipowasili kwenye Ukumbi wa Mikutano wa CCM wa Dodoma Convition Centre, uliopo njia ya Kuelekea Chuo Kikuu cha UDOM, Mjini Dodoma.* * Baadhi ya Wake wa Viongozi wakiwa kwenye Mkutano See more...............

Matukio ya jana usiku katika office za CCM: Mkutano Mkuu CCM waahirishwa hadi saa 4 asubuhi




12:43: Baada ya upigaji kura kwa wagombea wote watatu ili kumpata mmoja, Rais Jakaya Kikwete ameahirisha Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Taifa hadi saa nne asubuhi.


12:11 Mgombea wa mwisho wa CCM Dk John Pombe Magufuli amemaliza kujinadi mbele ya Mkutano mkuu wa CCM.


amesisitiza kuwa atakwenda kuilinda na kuisimamia ilani ya Chama cha Mapinduzi.


Amesema ataulinda Muungano na kuhakikisha kuwa anakisaidia Chama Cha Mapinduzi kupata ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi Mkuu wa mwezi Oktoba


12:01 Mgombea Dk Asha-Rose Migiro amemaliza kujinadi kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM akieleza hisia zake na nia yake thabiti ya kutaka kuliongoza taifa la Tanzania


Amesema atahakikisha anaulinda umoja wa kitaifa, kuulinda Muungano, Kuyalinda kipekee Mapinduzi ya Zanzibar, kupata Katiba Imara, pamoja na kusimamia yale yote yaliyomo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi.


11:51 Mgombea wa kwanza wa nafasi ya urais Balozi Amina Salum Ali ameanza kujinadi mbele ya wajumbe wa Mkutano mkuu wa CCM.


Amezungumzia suala la kulinda Muungano, kutekeleza yale mazuri na kuyatafutia ufumbuzi yale yote yaliyoachwa na Rais Kikwete. pia kusimamia majukumu ya chama imara kitakachokuwa na viongozi bora wanaosimamia maadili Serikalini.


Hakuulizwa swali lolote


11:37: Rais Jakaya Kikwete amemaliza kuzungumza na wajumbe wa mkutano mkuu mjini Dodoma akimfagilia Katibu Mkuu wa chama hicho Abdulrahman Kinana kwa madai kuwa amekifikisha chama katika eneo salama.


10: 59 Rais Jakaya Kikwete na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, anaanza kuzungumza na wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho


10:56 Mkutano Mkuu wa CCM umeanza mjini Dodoma na Muda huu Katibu Mkuu wa chama HichoAbdulrahman Kinana anazungumza. Pamoja na mambo mengine Anaeleza jinsi walivyoweza kufanya ziara katika mikoa yote nchi.read more,,,,,,,,,,,

Moshi mweusi watanda CCM



Moshi mweusi umezidi kukikumba Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya makada wa chama hicho wakiwemo wagombea urais kushindwa kuelewa ni nini kinachoendelea katika suala mzima la vikao vya kuwajadili na kuwachuja wanaowania kuteuliwa na chama kupeperusha bendera ya CCM.Hali hiyo imesababisha baad...hi ya wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) na wale wa Mkutano Mkuu kuendelea kujadili kinachoendelea kila wanapokutana kwenye vikundi na kwenye baa.Awali ilitarajiwa kwamba Kamati Kuu ingetangaza majina ya makada watano waliopitishwa kwa ajili ya kupelekwa kwenye NEC ili kupigiwa kura, lakini hali iliendelea kutawaliwa na ukimya mkubwa, huku wengi wakiwa hawajui kinachoendelea.Kwa mujibu wa ratiba iliyokuwa imetangazwa na CCM Kamati Kuu ilitarajiwa kumaliza kazi zake jana, lakini hadi saa mbili usiku, hakuna aliyekuwa akijua kinachoendelea.Baadhi ya wadadisi walisema ratiba tayari imevurugika, kwani baada ya kumalizika kikao cha Kamati ya Maadili, ilikuwa zamu ya Kamati Kuu kuja na majina hayo na kuondoa 33, lakini kinyume chake hali imezidi kuwa kimya.Habari ambazo zilipatikana mjini Dodoma jana, zilieleza kuwa Kamati Kuu ilitarajia kukutana mara baada ya Rais Kikwete kuvunja Bunge. Baada ya Bunge kuvunjwa waumini wa dini ya Kiislamu walienda kufuturu, huku kukiwa na uvumi kwamba kikao hicho kitafanyika baada ya kufuturu.Kwa mujibu wa vyanzo vyetu majina ya waliopitishwa na CCM kwa ajili ya kupelekwa kikao cha NEC yanatarajiwa kutangazwa leo majira

RAISE AND FAIL NDULI EDWARD LOWASSA , HIZI NI PICHA MBALI MBALI WAKIWA NA RAFIKI YAKE KIPENZI

kikulacho kiko nguoni mwako
Tokeo la picha la image of lowassa and kikwete

Wabunge Ukawa kuchagua mgombea urais



Dar es Salaam. Hatimaye leo wabunge wote wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wanakutana na viongozi wao wa jijini hapa kumchagua mgombea urais atakayeviwakilisha vyama hivyo katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25.


Mkutano huo wa wabunge umekuja baada ya vikao kufanyika mfululizo wiki hii, huku kukiwa na mvutano kuhusu nani au chama gani kisimamishe mgombea urais.


Jana gazeti hili liliripoti kwa uhakika habari zilizotoka ndani ya vikao hivyo na kuthibitishwa na Mwenyekiti mwenza wa Ukawa, Dk Emmanuel Makaidi, kuwa vyama hivyo vitaweka wazi mgombea wake wa urais leo.


“Tumeshakubaliana namna ya kugawana kata na majimbo 13 yaliyobaki na Jumamosi tutaweka wazi kwa wananchi. Pamoja na hilo pia tutamtangaza mgombea urais na chama anachotoka,” alisema Dk Makaidi.


Umoja huo umekuwa ukiongezeka nguvu tangu wakati wa mchakato wa Katiba mwaka jana, hali inayosababisha wafuasi wake kuamini kuwa yeyote atakayesimamishwa na umoja huo na kupigiwa kampeni kwa pamoja anaweza kujikuta anakuwa rais, mbunge au diwani.


Mvutano


Vikao vya umoja huo vilitawaliwa na mvutano baina ya wajumbe ndani ya umoja huo hasa katika nafasi ya mgombea urais baada ya kuwapo kwa watia nia zaidi ya mmoja.


Chanzo cha uhakika kutoka ndani ya umoja huo kilisema kuwa isingekuwa rahisi vikao vya namna hiyo vikakosa mvutano huo, kutokana na baadhi ya wajumbe kushindwa kukubaliana na vigezo vilivyowekwa tangu mikutano ya awali.


Iliilazimu Kamati Kuu ya Ukawa kufanya kazi ya ziada kuhakikisha kuwa maridhiano yanafikiwa ili kumpata mgombea, ndipo ikaamuliwa waalikwe wabunge wote wapige kura kupata mgombea.


Taarifa zaidi zilisema kuwa wajumbe walio wengi walikuwa wanaipa nguvu Chadema kutoa mgombea urais kutokana na nguvu yake hasa katika mikoa ya Bara, na ukweli kwamba tayari CUF imekwishapewa fursa hiyo Zanzibar.


Jana gazeti hili likinukuu vyanzo vya ndani ya kikao hicho, liliripoti kuwa licha ya kutangaza kugawana kata na majimbo yaliyobaki, jina la mgombea urais lingetangazwa leo endapo wajumbe wa Kamati Kuu ya Ukawa iliyokutana jana wangeafikiana.


Akihojiwa na kituo cha televisheni cha Azam jana, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa alisema leo vyama hivyo vitalitangazia dunia chama kipi kitatoa mgombea wa Ukawa.mwananchi

MCHAKATO URAIS CCM: Lowassa akatwa



Dodoma. “Anakatwa, hakatwi” ndilo swali lililokuwa linaulizwa nchi nzima jana, lakini hatimaye Kamati Kuu ya CCM iliyokutana hadi usiku wa manane iliibuka na jibu kwamba Edward Lowassa amekatwa, huku kukiwa na wingu zito baada ya wajumbe watatu kupingana na uamuzi huo.


Muda mfupi baada ya kikao hicho, pamoja na kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alikataa kutaja majina yaliyopitishwa, akaunti ya Twitter ya CCM, iliwataja waliopitishwa kuwa ni Bernard Membe, Dk John Magufuli, Dk Asha Rose Migiro, January Makamba na Amina Salum Ali na kuwatupa wengine 33 akiwamo Lowassa.


“Kikao cha Kamati Kuu kimeisha salama. Kesho (leo) Halmashauri Kuu itakutana kuanzia saa 4:00 asubuhi,” alisema Nape baada ya kikao hicho.


Alipotakiwa kutaja majina ya makada watano waliopitishwa, Nape alisema: “Nimeambiwa mchakato bado unaendelea na kesho (leo) Halmashauri Kuu itakutana kuendelea na kazi. Kwa hiyo nawakaribisha kesho kuanzia saa 4:00 asubuhi mje mchukue picha, habari, karibu sana.” Mkutano Mkuu utafanyika saa nane mchana leo.”


Dakika chache baada ya kikao hicho kumalizika, wajumbe watatu wa Kamati Kuu, wakiongozwa na mbunge wa Songea Mjini, Dk Emmanuel Nchimbi waliitisha mkutano na waandishi wa habari na kueleza kuwa wanapinga uamuzi huo ambao hawakuutaja, wakidai kuwa si majina yote yaliyowasilishwa mbele ya kamati hiyo.


Dk Nchimbi, akiongozana na mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Dodoma, Adam Kimbisa na mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Sofia Simba waliwaeleza waandishi wa habari mara tu baada ya mkutano wa Kamati Kuu kuwa kikao hicho hakikufuata kanuni kwa kuwa majina machache yaliwasilishwa na hayakuhusisha mgombea anayekubalika.


Ingawa hawakumtaja mgombea huyo waliyesema anatajwa na wengi, wajumbe hao wanafahamika kuwa wanamuunga mkono Lowassa.


Baada ya kikao hicho taarifa za wagombea hao zilisambaa kwa kasi katika mitandao ya kijamii na mijadala ya wazi ilianza kuhusu uamuzi wa kumtosa Lowassa, ambaye alikuwa Waziri Mkuu wa kwanza wa Serikali ya Awamu ya Nne.


Mmoja wa makada watano waliopitishwa kwenye mchujo huo aliithibitishia Mwananchi kuwa jina lake limepita, lakini akasema hataki akaririwe na badala yake akamshauri mwandishi aangalie akaunti ya twitter ya CCM baada ya nusu saa.


Habari za jina la Lowassa kukatwa zilizagaa tangu jana asubuhi, ilipoelezwa kuwa CCM ilifanya majadiliano na wadau mbalimbali kuangalia jinsi ya kudhibiti watu wanaounga mkono baada ya kupata taarifa kuwa ameenguliwa.


Lowassa azua mjadala


Awali wakati Kamati Kuu ya CCM ikikutana jana usiku kupitisha majina ya makada watano walioomba kuwania urais, jina la Edward Lowassa ndilo lililotawala mijadala mingi kwenye mitandao ya kijamii, likiambatana na swali moja; amekatwa, hajakatwa? chanzo gazeti la mwananchi

Dodoma kumekucha, Lowassa nje, matano yajulikana

Dodoma kumekucha, Lowassa nje, matano yajulikana

 

1:32 Tovuti ya CCM imeyatangaza majina matano yaliyopitishwa na Kamati ya CCM (CC) kuwa ni Bernard Membe, John Magufuli, Asha-Rose Migiro, January Makamba na Amina S Ali


12:55 Kikao cha Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CC) kimemalizika hivi punde mjini Dodoma na Katibu wa Itikadi na Ueneze Nape Nnauye ameshindwa kutaja majina matano ambayo yatapelekwa kwenye Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho (NEC)


Badala yake amewaambia waandishi wa habari kuwa majina hayo yatatangazwa saa nne asubuhi.


Aidha kwa mujibu wa Matangazo yaliyorushwa moja kwa moja na kituo cha redio Uhuru, Sophia Simba alisikika akisema kuwa mvutano mkali ulikuwemo ndani kikao hicho na wajumbe, Adam Kimbisa, Dk Emmanuel Nchimbi na yeye mwenyewe hawakukubaliana na maamuzi ya kikao yaliyofikiwa.


10:10 Bado kikao cha Kamati Kuu (CC) kinaendelea taarifa zilizopo ni kwamba kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kimeahirishwa hadi kesho saa nne asubuhi


8:12 Kikao cha Kamati Kuu kinarudi kuendelea na kitatoa taarifa ya majina matano ambayo kwa sababu ya muda yatajadiliwa kesho na Kikao cha Halmashauri na Mkutano Mkuu utafanyika kesho mchana, Kwa mujibu wa Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.



7:00 Kamati Kuu ya CCM imeeenda mapumziko mafupi kwa ajili ya Kufuturu na watarejea tena majira ya saa mbili usiku.


4:30 KUMEKUCHA Dodoma, Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeanza mkutano wake wa Kamati Kuu saa chache zilizopita.


Taarifa kutoka Dodoma zinasema watu wote wameondolewa ndani ukumbi mpya wa CCM ikiwa ni pamoja na waandishi wa habari ambapo hivi sasa wanasubiri taarifa hizo nje ya ukumbi huo.


Endelea kuwa nasi kwa habari zaidi kutoka Dodoma ......chanzo mwananchi

WASIRA ATINGA MAKAO MAKUU CCM KUCHUKUA FONU YA URAIS

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Stephen Wassira akikabidhiwa fomu ya kugombea urais.




Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Stephen Wassira akishuka kwenye Gari ili kuchukua fomu ya kugombea urais 2015 .




Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Stephen Wassira akiwasili ukumbini katika mkutano na Waandishi wa Habari leo. 


Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Stephen Wassira akisaini wakati wa kuchukua fomu ya kugombea urais paembeni ni mke wake.

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Stephen Wassira leo amekabidhiwa fomu ya kugombea urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi huku kipaumbele chake kikubwa kikiwa ni kuinua kilimo. 

Akizungumza na Waandishi wa Habari hivi sasa katika ukumbi wa mikutano wa makao makuu Wassira amesema ikiwa atachaguliwa kuwa rais ataboresha kilimo kwa kutumia zana za kisasa huku akisisitiza kuwa jembe la mkono litawekwa katika vyumba ya makumbusho ili iwe historia. 

Kwa upande wa ufisdi amesema ufisadi ni wizi,anausikia tu na kwa sababu atakuwa rais atahakikisha kuwa anawachukulia sheria pamoja na kuziongea nguvu sheria ili kupambana nao. 

Akizungumzia Muungano amesema atatetea na kuulinda maana kuuvunja ni kugawa nchi.

WAGOMBEA: Watano Kuchukua Fomu za Urais Leo.....Ataanza Mwandosya(Saa 4), Atafuata Wassira (Saa 5), Lowassa (Saa 7), Amina ( Saa 8) na Nyerere ( Saa 9)


Vumbi la kinyang’anyiro cha uteuzi wa kuwania urais ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), linaanza rasmi Dodoma leo kwa wanachama wake watano kuchukua fomu wakiomba uteuzi huo. 

CCM imepanga kuanzia leo Juni 3 hadi Julai 2, mwaka huu, kuwa siku za kuchukua na kurudisha fomu za wanachama wake wanaoomba uteuzi kuwania urais. 

Uteuzi huo ni kwa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, lakini kwa uteuzi wa Rais wa Zanzibar, fomu zitakuwa zikitolewa kisiwani Unguja. 

Tayari wanachama wa CCM kadhaa wamekwisha kutangaza nia ya kumrithi Rais Jakaya Kikwete huku wengine zaidi wakitarajiwa kufanya hivyo. 

Kwa mujibu wa Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) wa Oganaizesheni, Dk Muhammed Seif Khatib, uchukuaji wa fomu hizo unaanza rasmi leo. 

Khatib aliwaambia waandishi wa habari jana katika Makao Makuu ya CCM ‘White House’, Mtaa wa Nyerere mjini Dodoma kuwa fomu zitaanza kutolewa saa nne asubuhi. 

Alisema kwa mujibu wa orodha waliyonayo, wanachama watano watachukua fomu hizo kuanzia saa nne asubuhi hadi saa 10:30 jioni, na kila mmoja amepewa saa moja na wametenga muda wa kuzungumza na waandishi wa habari kwa wagombea ambao wataona inafaa kwao. 

“Uchukuaji huu wa fomu haukufuata umaarufu wa mtu, ujuzi, alfabeti, nafasi yake katika Chama na Serikali, bali umefuata aliyewahi kutoa taarifa kwa Chama,” alisema Khatib akifafanua uchukuaji huo. 

Alimtaja wa kwanza kuchukua fomu kuwa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Mark Mwandosya kuanzia saa 4 kamili hadi saa 5:30. 

Profesa Mwandosya atafuatiwa na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Stephen Wassira kuanzia saa 5:30 na atafuata Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa atachukua fomu kuanzia saa saba kamili. 

Wa nne atakuwa Waziri wa zamani wa Muungano, Balozi Amina Salum Ali kuanzia saa 8:30 mchana na pazia la ufunguzi litafungwa saa 9:30 alasiri na mtoto wa Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, Charles Makongoro Nyerere. 

Mbali ya wanachama hao watano, wanaCCM wengine ambao wametangaza nia ya kuwania urais ni Lazaro Nyalandu, Frederick Sumaye, Profesa Sospeter Muhongo, January Makamba, Mwigulu Nchemba na Luhaga Mpina. 

Wanaotajwa ni pamoja Bernard Membe, William Ngeleja, Dk Titus Kamani, Luhaga Mpina, Mizengo Pinda, Dk Asha-Rose Migiro, Shamsi Vuai Nahodha, Dk Emmanuel Nchimbi na Dk Hamis Kigwangalla. 

Katibu huyo wa Oganaizesheni alisema uchukuaji huo wa fomu utazingatia taratibu zilizowekwa na CCM na kutakuwa na fomu tatu zitakazopewa wagombea. 

“Fomu ya kwanza itahusu maelezo binafsi ya mgombea, itahusu uzoefu na ujuzi wake, nyingine itakuwa ya kujaza orodha ya wadhamini wake na nyingine ya masharti kama yalivyokubaliwa na Halmashauri Kuu ya Taifa,” alifafanua Dk Khatib. 

Alisema katika wadhamini, mgombea atatakiwa kupata wadhamini 450 kutoka katika mikoa 15 ya Tanzania Bara na mikoa mingine mitatu ya Tanzania Zanzibar. 

“Mjumbe yeyote wa Mkutano Mkuu wa Taifa haruhusiwi kumdhamini mgombea, pia mwanachama haruhusiwi kudhamini mgombea zaidi ya mmoja,” alifafanua. 

Alisema ili kuonesha uhalali wa fomu hizo za wadhamini, zitapaswa kuwa na mhuri wa Katibu wa CCM wa wilaya husika pamoja na saini yake na pia mdhamini atapaswa kusaini na kuandika kadi yake ya uanachama. 

Alisema wagombea hao watakapofika kuchukua fomu, wanapaswa kuwa na ada ya Sh milioni moja na watasaini daftari maalumu kuonesha ndio waliochukua fomu. 

“Tumepanga muda wa saa moja moja na nusu kwa kila mgombea kuwapo hapa. Na akishachukua fomu tumepanga anayetaka azungumze na waandishi wa habari kwenye Ukumbi wa NEC,” alisema Dk Khatib. 

Alisema katika chumba cha uchukuaji wa fomu, wataruhusiwa mgombea kuingia na watu wasiozidi 10. 

“Katika chumba hiki (cha mikutano na waandishi katika Makao Makuu) tutaruhusu mgombea kuingia na watu wasiozidi 10… mkewe na jamaa zake wengine, wanaomsindikiza, sijui wengine mnawaita wapambe, mimi nawaita wanaomsindikiza,” alisema Katibu huyo. 

Aliwataka wagombea wengine wanaotaka kuchukua fomu hizo kuwasiliana mapema na ofisi yao kwani alisema wangependa kazi ya uchukuaji fomu kudumu kwa siku zisizozidi tano ili shughuli nyingine ziendelee. 

“Tunawaomba wagombea wengine wanaotaka kuja kuchukua fomu kufanya hivyo mapema. Tungependa ndani ya siku tano tuwe tumemaliza ili shughuli nyingine ziendelee kwani hata wao wana kazi ya kutafuta wadhamini mikoani,” alifafanua kiongozi huyo mkongwe.

MABADILIKO MENGINE KUHUSU UCHAGUZI MKUU BURUNDI!!


Hali bado si shwari Burundi..hii inatokana na machafuko ya kisiasa yanayoendelea baada ya Rais aliyeko madarakani Pierre Nkurunziza kutaka kuwania kwa muhula wa tatu mfululizo. 

Baada ya kutofikia makubaliano ikiwemo jaribio la kutaka kumpindua lililofanywa kushindikana huku watu wakiendelea kaadamana kushinikiza aondoke. 

Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amehairisha uchaguzi wa ubunge kwa siku kumi . 

Msemaji wa rais Willy Nyamitwe amesema Rais huyo ameahirisha uchaguzi wa Ubunge kwa muda wa siku 10 kufuatia jaribio la mapinduzi. 

Awali uchaguzi huo ulipangwa kufanyika Mei 26 na sasa utafanyika June 2 na umeahirishwa ili kupata muda wa kuwasikiliza washirika wa kimataifa pamoja na tume ya uchaguzi. 

Hadi sasa tarehe rasmi ya uchaguzi wa Urais uliopangwa kufanywa Juni 26 haijabadilika
-BBC
Older Posts
© Copyright WORLD OF TODAY Published.. Blogger Templates
Back To Top